Friday, 5 June 2020

HISTORIA FUPI YA UBAGUZI WA RANGI NCHINI MAREKANI


HISTORIA YA UBAGUZI WA RANGI AMERIKA (MAREKANI)

Ubaguzi wa rangi ni kitendo cha/imani ya kumbagua/kumtenga/kumchukia mtu kwa misingi ya asili yake na rangi ya ngozi yake. Hii sio kitu kigeni sana na ni vigumu kusemea kirahisi ni lini hasa ubaguzi wa rangi ulianza hasa kabla ya karne ya 15. Wakati wazungu wanakuja Afrika kwa mara ya kwanza kutoka Ureno (Portugal) walidhan kua Waafrika ni jamii hasimu kwao kwa maana ina uwezo sawa na wao lakini punde wakajua waafrika walikua dhaifu kwenye baadhi ya maeneo na hapo waafrika wakaanza kuchukuliwa jamii dhaifu (Inferior race). Hali hii ndio iliopelekea kuzaliwa kwa biashara haram na ya kishenzi_biashara ya utumwa.