Saturday, 20 May 2017

WATU WALIOKATALIWA KUISHI NCHI KAVU.


Wabajui huishi na familia zao kwenye vibanda vyao vya miti vilivyojengwa baharini kwani wamezuiwa kuishi nchi kavu na pia pia wakikaa sana nchi kavu wanajihisi kuumwa. 

Dunia ina mambo mengi sana, mengine yanastaajabisha, mengine kuudhi na mengine kufurahisha. Ila hili sijui linaleta picha gani.
Bahari ni makazi ya karibu nusu ya viumbe hai waishio duniani ila sisi binadamu sio mojawapo ya viumbe hivyo kwani hatuwezi kukaa ndani ya maji ya chumvi kwa   muda mrefu, hatuwezi kuzama na kukaa kwenye kina cha bahari kwa muda mrefu lakini kinyume na haya yote kuna baadhi ya binadamu karibia maisha yao yote ni baharini! Wamejenga "vijumba/vibanda" vyao vya miti huko na asilimia zaidi ya 90 wanaishi huko na sio nchi kavu! Naam, ni watu jamii ya

Sunday, 14 May 2017

KOREA KASKAZINI YAFYATUA KOMBORA JIPYA.

Google
Uwezo wa makombora yanayomilikiwa na Korea kaskazini. 

Korea kaskazini imerusha kombora jingine mapema leo jumapili ambalo liliruka karibu 700km, hayo ni kwa mujibu wa jeshi la Korea kusini. Hayo yanajiri ikiwa ni siku chache tu tangu rais mpya wa Korea kusini kushika wadhifa wa urais hapo jumatano. Rais mpya wa Korea alisisitiza kua yuko tayari kufanya mazungumzo na utawala wa Pyongyang kama mazingira yataruhusu.

MTOTO WA OSAMA BIN LADEN AAPA KULIPA KISASI

Mmoja kati ya watoto wa aliyewahi kua kiongozi wa kundi la Al qaeda ameapa kulipa kisasi cha mauaji ya baba yake yaliyotekelezwa na kikosi cha makomando wa kimarekani mwaka 2013 nchini Afganistani. 
Picha hii ilipigwa na kituo cha televisheni cha Al jazeera japo haifahamiki ilikua ni lini. 

Mtoto wa Osama bin laden anasemekana kua anapanga kufanya mashambulizi ya kulipiza kisasi juu ya kifo cha baba yake kilichotokea May 2013. Mtoto huyo pia (Hamza) anajiandaa kua kiongozi mpya wa kundi la Al Qaeda.