HAMAS: KUTOKA KIKUNDI CHA KUTOA MISAADA MPAKA KIKUNDI CHA KISIASA NA KIJESHI.
Ili kuelewa
imani na itikadi kali ya Hamas kabla hata kuundwa kwake tuone kidogo ikitikadi ya
Waarabu juu ya taifa la Israel hasa kabla ya vita vya siku sita [5-11 June
1967]. Hizi ni kauli za kukupa picha HAMAS wanasimamia nini na Wanapigania nini.
Radio
Cairo ilitangaza kua "[Watu] Waarabu wamedhamiria kikamilifu kuifuta
Israel katika ramani na kirejesha heshima ya watu wa Palestina". May 25,
1967.
May
28, 1967 rais wa Misri Gamal Abdel Nasser anasema "Hatutakubali uwezekano wowote ule wa
Israel na Palestina kuwepo pamoja".
31
May 1967 rais wa Iraq Abdel Rahman Aref anasema "Uwepo wa Israel ni dosari
ambayo ni lazima irekebishwe".
Utaona
msimamo mkali wa Waarabu dhidi ya Israel kwa hio salama ya Israel ilikua ni
kupitia kujua namna gani atakua wa kwanza kujilinda dhidi ya maadui zake ambao
wote wanatangaza kumuangamiza.
Sasa
kwanini HAMAS ilianzishwa turudi 29 August 1967 kule Khartoum Sudan kulikaliwa
mkutano wa Shirikisho la nchi za Kiarabu (Arab League) iliokua na makao makuu
pale Cairo, Misri. Katika kilele cha mkutano huo Arab League ilikuja na azimio
la HAKUNA/HAPANA TATU (THREE NOES) ikiwa ni No peace with Israel, No
recognition of Israel na No negotiation with Israel [ Hakuna amani na Israel,
Hakuna kuitambua Israel na Hakuna majadiliano na Israel]. Na hili linaanzia
katika imani ya Waarabu hata kabla ya vita mfano tizama msimamo wa Misri na
Iraq kabla ya June 5, 1967.
:::::::::::::***