MGOGORO WA ISRAEL NA PALESTINA-3
HAMAS: KUTOKA KIKUNDI CHA KUTOA MISAADA MPAKA KIKUNDI CHA KISIASA NA KIJESHI. Jeshi la Israel Ili kuelewa imani na itikadi kali ya Hamas kabla hata kuundwa kwake tuone kidogo ikitikadi ya Waarabu juu ya taifa la Israel hasa kabla ya vita vya siku sita [5-11 June 1967]. Hizi ni kauli za kukupa picha HAMAS wanasimamia nini na Wanapigania nini. Radio Cairo ilitangaza kua " [Watu] Waarabu wamedhamiria kikamilifu kuifuta Israel katika ramani na kirejesha heshima ya watu wa Palestina" . May 25, 1967. May 28, 1967 rais wa Misri Gamal Abdel Nasser anasema " Hatutakubali uwezekano wowote ule wa Israel na Palestina kuwepo pamoja ". 31 May 1967 rais wa Iraq Abdel Rahman Aref anasema " Uwepo wa Israel ni dosari ambayo ni lazima irekebishwe". Utaona msimamo mkali wa Waarabu dhidi ya Israel kwa hio salama ya Israel ilikua ni kupitia kujua namna gani ataku...