Wednesday, 3 August 2016
RAISI AMTEUA MKEWE KUA MGOMBEA MWENZA
Managua. Rais wa Nicaragua, Daniel Ortega amemtaja mkewe kama mgombea mwenza na makamu wa rais wakati huu ambapo anawania kuchaguliwa kwa muhula mwingine.
Tuesday, 2 August 2016
WATAWALA WA SHERIA AU UTAWALA WA SHERIA??
UTAWALA WA SHERIA vs WATAWALA WA SHERIA.
Hiki kichwa cha habari niliona kikiwa kwenye lugha ya kingereza. Ni kitabu kilichoandikwa na Prof. Issah Shivji akielezea maisha ya Jaji mkuu mstaafu Barnabas Albert Sammata. Nilipenda kukisoma kitabu hiki lakini sikufanikiwa. Ila nilifanikiwa kupata dhima ya juu ya kitabu. Lakini nilipenda maneno machache tu ya jaji samata ambayo nami ntayatumia hapa.
Aliwahi kusema "Let everyone in our society give justice a chance to prevail".(Hebu tufanye kila mmoja wetu katika jamii aipe haki nafasi ya kukua"[tafsri sio rasmi]).
Katika taifa lolote lile litakalokua linajiita ni taifa la kidemokrasia basi halina budi kuruhusu ustawi wa haki. Na haki itakuepo pale tu ambapo watu waliopewa dhamana ya kuisimamia wanakua na maadili. Amini usiamini ila kuna kazi hazihitaji saana maadili kama zingine.
Uongozi ni kazi ambayo huwezi kuifanya kama huna maadili. Wanasaikolojia wanaamini ili kuweza kumjua mtu alivyo ni lazma tumjue kupitia tabia. Tabia ni matendo ya nje ya mtu yanayodhihirisha namna alivyo kwa ndani(fikra, maono,imani yake ya ndani). Sasa mtu anachokiongea na kukifanya kwa dhamira jua ndivyo alivyo(awazavyo mtu ndivyo alivyo).
Sasa basi tumeshaona matendo ya viongozi wetu, wameonesha dhamira zao za ndani, imani na mitazamo yao imeoneshwa kwa kauli na matendo yao. Mwanzo nilidhani ni mapitio lakini sasa naamini ni dhamira zao. Hadi sasa kuna nafasi finyu ya kusema demokrasia haijateteleka; utawala wa sheria unaheshimiwa. Ni rahisi kusema kuna utawala wa sheria lakini utapata shida kudhihirisha kwani mifano halisi iliyopo inapingana na demokrasia; inapingana na utawala wa sheria. Karne hii ni karne ya kuzuia Bunge(chombo cha wananchi) kurusha matangazo ya papo kwa hapo? Kuwakataza na au kuwahukumu mawakili wanaohitolea kuwatetea wananchi? (c'mon tuko serious kiasi gani??), kuzuia mikutano ya kisiasa kwa sababu ambazo kwa akili ya kawaida zina walakini. Taifa limetumbukia kwenye tatizo kubwa la kauli reja reja! Kauli hazina msingi wala nguzo ya kikatiba au kisheria. Haijalishi tunatamani maendeleo kwa kiasi gani lakini isiwe ndio tiketi ya kuangamiza utu na uhuru wa mwananchi, isiwe ndiyo tiketi ya dhulma na utawala usiofuata sheria. Kwa yanayoendelea nalazimika kuamini kua kwa sasa tayari kuna watu wanaogopwa na sheri(kuna mazingira sheria inaogopa watu). Naamini bado kuna upofu wa kisiasa. Tujue na tulmelewe kabisa kua siasa na maisha havitenganishwi hata kidogo. Kauli ya kiongozi wa kisiasa ina athari kubwa kwa jamii kwani wao wana ushawushi kwa watu wao hivyo kauli yeyote iliyokinyume na matakwa ya jamii husika ni wazi kua italeta madhara hasi nengi na mwisho wa siku labda litapelekea 'anguko la kijamii'. Kupitia kauli utapanda chuki au upendo, utapanda wema au uovu, utapanda woga au kujiamini. Na falsafa ya maisha na uongozi wa sasa ndio falsafa ya viongozumi wa baadae kwani ndicho kinachojengeka akilini mwa watu wa sasa.
Ila naanini historia inakwenda kwa mfumo wa mawimbi(waves). Na siku zote tunasoma historia lakini hatuelewi. Tulipaswa kujifunza kupitia historia ili kutoruhusu makosa yale yale kurudiwa katika hali na mazingira yale yale.Na hii tabia ya historia inafanya historia kujirudia. Nakumbuka historia ya Adolf Hittler alipoitwaa ujerumani rasmi mwanzoni mwa 1930s, nakumbuka mengi na makubwa aliyafanya ila mwisho wa siku alijichimbia kaburi na kuiacha Ujerumani ikiwa kama mkiwa huku ikinyoshewa vidole vya ubaya.
Hakuna namna yoyote sisi tunaweza kujisifu kua tumepiga hatua katika demokrasia. Bado tungali tumenasa katika tope la fikra zilizofubaa; mawazo mgando na mitazamo hasi. Tunakimbia mbio kuelekea uelekeo tusioujua tukiamini kua kutafika salama! Hivi ni nani aliyeturoga?? Mchawi wa kwanza ni mimi(ninayesoma hapa). Na hatuna cha kujivuna kama maendeleo yetu yatakua juu ya kafara za watu wetu. Ulishawahi jiuliza nani aliifanya North America na Ulaya kua kama ilivyo leo?? Nabi alikua kafara??
Demokrasia ya danganya toto na ya woga ndiyo iliyotawala barani Afrika hadi nashangaa kuona pia baadhi ya ya watu wakiiona nchi yetu kama nchi iliyopiga hatua kidokrasia. Na yeyote aitazamaye Tanzania kama nchi iliyokomaa kidemokrsia basi yeye na taifa lake watakua wametumbukia katika lindi la mauti ya fikra, wanaishi kwa fikra mfu na huo ni mwanzo wa anguko la nchi hiyo katika dhambi ya dhuluma ya haki kwa maana huwezi kubali kipofu kuongoza njia tena akiwa hana kifaa chochote. Huo ni uchawi. Sasa hatuwezi ongoza taasisi au nchi kwa kutumia mazingaombwe. Lazima tujikane tuoneshe dhamira zetu za ukombozi kwa kuheshimu haki na utu wa mtu. "Maendeleo ya vitu bila mtu ni upuuzi na batili". Na hakuna maendeleo bila HAKI NA UHURU. Haki na Uhuru ndo viungo thabiti vya dhana nzima ya maendeleo. Acha watu wawe huru na ukiwa huru utaishi kwa amani. Ni muda wa kuanza kufikiri upya, ni muda wa kujitathimini, kujikosoa na kujisahihisha. Tunahitaji maendeleo ya vitu na watu. Kuna faida gani kua na shule, hospitali zilizo kama magereza? Kuna faida gani kua na barabara nzuri kama tutakua hatupiti? Fikiria nje ya sanduku nyeusi(Black box).
Hiki kichwa cha habari niliona kikiwa kwenye lugha ya kingereza. Ni kitabu kilichoandikwa na Prof. Issah Shivji akielezea maisha ya Jaji mkuu mstaafu Barnabas Albert Sammata. Nilipenda kukisoma kitabu hiki lakini sikufanikiwa. Ila nilifanikiwa kupata dhima ya juu ya kitabu. Lakini nilipenda maneno machache tu ya jaji samata ambayo nami ntayatumia hapa.
Aliwahi kusema "Let everyone in our society give justice a chance to prevail".(Hebu tufanye kila mmoja wetu katika jamii aipe haki nafasi ya kukua"[tafsri sio rasmi]).
Katika taifa lolote lile litakalokua linajiita ni taifa la kidemokrasia basi halina budi kuruhusu ustawi wa haki. Na haki itakuepo pale tu ambapo watu waliopewa dhamana ya kuisimamia wanakua na maadili. Amini usiamini ila kuna kazi hazihitaji saana maadili kama zingine.
Uongozi ni kazi ambayo huwezi kuifanya kama huna maadili. Wanasaikolojia wanaamini ili kuweza kumjua mtu alivyo ni lazma tumjue kupitia tabia. Tabia ni matendo ya nje ya mtu yanayodhihirisha namna alivyo kwa ndani(fikra, maono,imani yake ya ndani). Sasa mtu anachokiongea na kukifanya kwa dhamira jua ndivyo alivyo(awazavyo mtu ndivyo alivyo).
Sasa basi tumeshaona matendo ya viongozi wetu, wameonesha dhamira zao za ndani, imani na mitazamo yao imeoneshwa kwa kauli na matendo yao. Mwanzo nilidhani ni mapitio lakini sasa naamini ni dhamira zao. Hadi sasa kuna nafasi finyu ya kusema demokrasia haijateteleka; utawala wa sheria unaheshimiwa. Ni rahisi kusema kuna utawala wa sheria lakini utapata shida kudhihirisha kwani mifano halisi iliyopo inapingana na demokrasia; inapingana na utawala wa sheria. Karne hii ni karne ya kuzuia Bunge(chombo cha wananchi) kurusha matangazo ya papo kwa hapo? Kuwakataza na au kuwahukumu mawakili wanaohitolea kuwatetea wananchi? (c'mon tuko serious kiasi gani??), kuzuia mikutano ya kisiasa kwa sababu ambazo kwa akili ya kawaida zina walakini. Taifa limetumbukia kwenye tatizo kubwa la kauli reja reja! Kauli hazina msingi wala nguzo ya kikatiba au kisheria. Haijalishi tunatamani maendeleo kwa kiasi gani lakini isiwe ndio tiketi ya kuangamiza utu na uhuru wa mwananchi, isiwe ndiyo tiketi ya dhulma na utawala usiofuata sheria. Kwa yanayoendelea nalazimika kuamini kua kwa sasa tayari kuna watu wanaogopwa na sheri(kuna mazingira sheria inaogopa watu). Naamini bado kuna upofu wa kisiasa. Tujue na tulmelewe kabisa kua siasa na maisha havitenganishwi hata kidogo. Kauli ya kiongozi wa kisiasa ina athari kubwa kwa jamii kwani wao wana ushawushi kwa watu wao hivyo kauli yeyote iliyokinyume na matakwa ya jamii husika ni wazi kua italeta madhara hasi nengi na mwisho wa siku labda litapelekea 'anguko la kijamii'. Kupitia kauli utapanda chuki au upendo, utapanda wema au uovu, utapanda woga au kujiamini. Na falsafa ya maisha na uongozi wa sasa ndio falsafa ya viongozumi wa baadae kwani ndicho kinachojengeka akilini mwa watu wa sasa.
Ila naanini historia inakwenda kwa mfumo wa mawimbi(waves). Na siku zote tunasoma historia lakini hatuelewi. Tulipaswa kujifunza kupitia historia ili kutoruhusu makosa yale yale kurudiwa katika hali na mazingira yale yale.Na hii tabia ya historia inafanya historia kujirudia. Nakumbuka historia ya Adolf Hittler alipoitwaa ujerumani rasmi mwanzoni mwa 1930s, nakumbuka mengi na makubwa aliyafanya ila mwisho wa siku alijichimbia kaburi na kuiacha Ujerumani ikiwa kama mkiwa huku ikinyoshewa vidole vya ubaya.
Hakuna namna yoyote sisi tunaweza kujisifu kua tumepiga hatua katika demokrasia. Bado tungali tumenasa katika tope la fikra zilizofubaa; mawazo mgando na mitazamo hasi. Tunakimbia mbio kuelekea uelekeo tusioujua tukiamini kua kutafika salama! Hivi ni nani aliyeturoga?? Mchawi wa kwanza ni mimi(ninayesoma hapa). Na hatuna cha kujivuna kama maendeleo yetu yatakua juu ya kafara za watu wetu. Ulishawahi jiuliza nani aliifanya North America na Ulaya kua kama ilivyo leo?? Nabi alikua kafara??
Demokrasia ya danganya toto na ya woga ndiyo iliyotawala barani Afrika hadi nashangaa kuona pia baadhi ya ya watu wakiiona nchi yetu kama nchi iliyopiga hatua kidokrasia. Na yeyote aitazamaye Tanzania kama nchi iliyokomaa kidemokrsia basi yeye na taifa lake watakua wametumbukia katika lindi la mauti ya fikra, wanaishi kwa fikra mfu na huo ni mwanzo wa anguko la nchi hiyo katika dhambi ya dhuluma ya haki kwa maana huwezi kubali kipofu kuongoza njia tena akiwa hana kifaa chochote. Huo ni uchawi. Sasa hatuwezi ongoza taasisi au nchi kwa kutumia mazingaombwe. Lazima tujikane tuoneshe dhamira zetu za ukombozi kwa kuheshimu haki na utu wa mtu. "Maendeleo ya vitu bila mtu ni upuuzi na batili". Na hakuna maendeleo bila HAKI NA UHURU. Haki na Uhuru ndo viungo thabiti vya dhana nzima ya maendeleo. Acha watu wawe huru na ukiwa huru utaishi kwa amani. Ni muda wa kuanza kufikiri upya, ni muda wa kujitathimini, kujikosoa na kujisahihisha. Tunahitaji maendeleo ya vitu na watu. Kuna faida gani kua na shule, hospitali zilizo kama magereza? Kuna faida gani kua na barabara nzuri kama tutakua hatupiti? Fikiria nje ya sanduku nyeusi(Black box).
Monday, 1 August 2016
Sunday, 31 July 2016
JARIBIO LA KUKUONESHA KAMA HUYO ULIYE NAYE ATAKUA MME MZURI KWAKO.
Jaribio muhimu kujua kama kweli atakua mume mwema kwako.
Ndoa ni safari ndefu na ni muhimu kwa watu kuchagua wenza wao wa maisha ili waweze kuishi nao. Kuna maswali muhimu unapaswa kujiuliza kuhusu huyo mme wako wa baadae ili kujua mahusiano yenu yanaweza kwenda mbali kiasi gani. Kuna viashiria vinaweza kukuonesha ni kipi unaweza kukipata baada ya wewe kumkubali huyo uanaemfikiria kua awe mmeo.
Ndoa ni safari ndefu na ni muhimu kwa watu kuchagua wenza wao wa maisha ili waweze kuishi nao. Kuna maswali muhimu unapaswa kujiuliza kuhusu huyo mme wako wa baadae ili kujua mahusiano yenu yanaweza kwenda mbali kiasi gani. Kuna viashiria vinaweza kukuonesha ni kipi unaweza kukipata baada ya wewe kumkubali huyo uanaemfikiria kua awe mmeo.
Subscribe to:
Posts (Atom)