BAADA YA MIAKA 113 KANISA LAHAMISHWA BILA KUVUNJWA.
Kanisa la Lutheran la Kiruna huko Sweeden likiwa tayari kusafirishwa. Picha kwa hisani ya Forbes Katika hali ambayo sio ya kawaida kanisa moja la kihistoria huko nchini Sweeden limehamishwa kutoka sehemu mabo lilijengwa na kupelekwa sehemu nyingine baada ya miaka 113 la kuwepo katika eneo ambapo ujenzi wake ulikamilika mwaka 1912. Kuhamishwa kwa kanisa hilo la Lutheran ni kutokana na kuwepo kwa uchimbaji wa madini ya chuma chini ya kanisa hilo na maeneo mengine ya jirani. Mpango wa kuhamisha kanisa hilo bila kubomoa umekua ukiendelea kwa takribani mwaka mmoja ambapo wataalam wamekiri kwamba haikua kazi rahisi.