Posts

Showing posts from August 24, 2025

TRUMP NA MAREKANI VS NICOLAS MADURO NA VENEZUELA, JE, VITA IKO KARIBU?

Image
Rais wa Venezuela Nicholas Maduro. Picha na Reuters  Kumekuwapo na sintofahamu kubwa juu ya kile kinachoendelea kati ya Marekani na Venezuela kufuatia matendo hatarishi ya pande zote mbili. Awali Marekani ilitangaza dau nono la dola milioni 50 ambazo ni sawa na karibu sawa na shilingi 12, 529, 390, 000/= kama zawadi kwa mtu yeyote anatakaye wezesha kupatikana na kukamatwa kwa Rais wa Venezuela ambae anatuhumiwa kwa ulanguzi wa madawa ya kuelevya. Lakini hilo limechukua sura mpya baada ya Marekani kutuma meli za kivita pamoja na nyambizi karibu na Venezuela kitu ambacho kimemlazimu Rais Maduro kuanza kukusanya wanajeshi wakijiandaa kwa makabiliano ikiwa Marekani itawavamia. 

UEFA IMEFANYA MABADILIKO YA MUDA WA KUCHEZA SIKU YA FAINALI

Image
Shirikisho la mpira barani Ulaya linalosimamia mashindano ya Ligi ya mabingwa Ulaya kwa maana ya UEFA wametangaza mabadilko katika muda wa mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kuanzia msimu huu ya 2025/2026 ambayo itachezwa pale katika uwanja wa Puskas huko Budapest nchini Hungari. Mabadiliko haya ya muda yanafuatia tathmini ambayo UEFA wameifanya na kuamua kuweza kuwapa burudani mashabiki ambao hapo awali wamekua wakisumbuka kutokana na mechi baadhi kuchelewa kuisha hasa pale michezo hiyo inapoenda katika muda wa nyongeza na mikwaju ya penati. 

TOP 10 YA SIMU ZENYE KAMERA BORA ZAIDI DUNIANI MPAKA SASA

Image
Picha za smartphone mbalimbali Miongoni mwa masoko magumu kwa sasa ni pamoja na soko la simu janja au rununu (smartphones) ambapo kila kampuni ya utengenezaji wa siku inajitajidi kutoa simu zenye ubora wa hali ya juu. Lakini sio rahisi kama unavofikiria ikiwa utaulizwa ipi ni simu bora kwa sasa sokoni. Kwa sababu simu moja kutoka kampuni flani inaweza kua bora kwenye eneo moja au mawili hivi lakini ikashindwa kua bora katika maeneo mengine. Lakini kati ya vitu virahisi na hua ni kigezo cha watu kununua simu hua ni kamera. Hii hapa ni orodha ya simu 10 zenye kamera bora sana mpaka sasa. 

IRAN NA ULAYA ZAINGIA KATIKA MZOZO MPYA HUKU MAREKANI IKITAJWA PIA.

Image
Kiongozi mkuu wa taifa la Iran Ayatollah Ali Khamenei. Picha na New York Times Ni takribani miezi miwili imepita tangu kumalizika kwa vita vya siku 12 kati ya Israel na Iran. Katika vita hivyo ilishuhudiwa pia Marekani akiingilia kati kwa kuvishambulia vinu muhimu ya Nyuklia vya Iran ikiwemk kile kinu kikubwa zaidi cha Fordow, Nantaz na Isfahan tarehe Juni 22, 2025 ambapo mashambulizi hayo yaliibua hisia mseto kutoka katika Jumuiya ya kimataifa. Kufuatia mashambulizi hayo Trump alisema wameharibu kabisa uwezo wa Nyuklia wa Iran na kwamba huo ulikua ni ushindi mkubwa sana kwa usalama wa dunia. Lakini kauli ya Trump inapingana na ripoti ya shirika la ujasusi wa kiusalama lililo chini ya Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) yaani Defense Intelligence Agency(DIA). Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali ambayo kulingana na unyeti wa taarifa hawakutaka kutajwa walisema mashambulizi katika vinu vya nyuklia huko Iran vilirudisha nyuma mpango wa Nyuklia wa Iran kwa miezi kadhaa tu nyuma. Wakiamini ...

YOUTUBE ILITUMIA AKILI UNDE (AI) KUHARIRI VIDEO ZA WATU KWA SIRI

Image
Picha na AFP/Getty Images  Akili unde (AI) kama inavyofahamika imekua ni mapinduzi makubwa katika sayansi na teknolojia na kwa sasa ni ngumu kuwaza dunia bila Akili unde. AI sasa hivi inatumika katika tafiti za kisayansi, elimu, afya, viwandani, mtandaoni na karibu kila nyanja ya maisha ya binadamu kuna matumizi ya Akili Unde (AI) kwa kiasi fflani. Licha ya kua na fursa nyingi bado AI imeacha mwanya wa changamoto hasa zile zinazohusu hatimiliki na uhalisia wa mawazo au ubunifu kwani kam kitu au wazo litku limesanifiwa na akili unde ni ngumu kudai kwamba ni wazo lako licha ya kwamba uliielekeza namna ya kufanya. Katika changamoto mojawaponkubwa sasa inaikumba kampuni ya Google kupitia bidhaa yake ya YouTube.

MAANDAMANO MAKUBWA HUKO ISRAEL KUMSHINIKIZA NETANYAHU KUMALIZA VITA

Image
Mtu akionekana kuvuka barabara ambapo matairi yalichokwa moto siku ya maandamano Jumanne 26 Agosti 2025. Picha na Times of Israel/Idit Avishay/Pro Democracy Protest Movement  Maandamano makubwa yamefanyika leo kote  nchini Israel ambapo waandamanaji wamezuia barabara zote muhimu katika jiji la Tel Aviv wakiwa na lengo la kuishinikiza serikali ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kukomesha vita huko ukanda wa Gaza na kuweka kipaumbele kuachiwa kwa mateka wa Israel ambao bado wangali wanashikiliwa na wanamgambonwa Hamas huko Gaza. Maandamano hayo yamendaliwa na kuratibiwa na Hostages and Missing Families Forum.  Waziri mkuu wa Israel anakaniliaa na shinikizo kubwa la umma kufuatia vita ambavyo ukomo wake bado haufahamiki huko Gaza. Hayo yanajiri huku pia kukiwa na msukumo wa jumuiya ya kimataifa wa kumtaka Netanyahu kuamaliza vita vya Gaza vilivyodumu kwa takribani miezi 22 hadi sasa. Jana serikali ya Israel ilikuri kufanya shambulizi katika hospitali ya Nasser huko Gaza ambap...

TAJIRI WA DUNIA VITANI TENA JUU YA AI. MUSK AZISHTAKI APPLE NA OPEN AI

Image
Picha kwa hisani ya mtandao  Mwishoni mwa wiki iliyopita niliandika kuhusu Open AI kumkaanga Elon Musk na Mark Zuckerberg juu ya kutaka kuiua kampuni chipukizi ya Open AI ambayo inamiliki programu maarufu ya ChatGPT. Na jana Jumatatu tunashuhudia kesi nyingine inayovutia miongoni mwa wataalamu wa kesi za teknolojia kwani tajiri namba moja duniani, Elon Musk amezishtaki kampuni za Apple na Open AI kwa kujimilikisha soko la Akili Unde (AI). Kwa mujibu wa Elon Musk Apple na Open AI ambao wanamiliki 65% ya soko la simu Marekani na 85% ya Chat bot huko Marekani mtawalia wamejimilikisha soko la huduma na kufanya iwe vigumu kwa kampuni nyingine kama vile xAI ambayo inaimiliki Grok kushindwa kushindana katika hali ya usawa. 

DONALD TRUMP KUKUTANA NA KIM JONG UN TENA?

Image
           Rais Kim Jong Un wa Korea Kaskazini na Donald Trump wa   Marekani               walipokutana kwenye mpaka wa Korea Kaskazini na Korea Kusini 2019. Picha na Reuters Korea Kaskazini na Korea Kusini hazijawahi kuaa na mahusiano mazuri kwa historia ya hivi karibu na hilo ni sawa sawa kwa uhusiano kati ya Korea Kaskazini na Narekani. Korea Kaskazini ni miongoni mwa chache duniani ambazo zimetengwa zaidi na zenyewe zinajitenga na dunia nyingine. Ni nadra kuona mikutano ya kidiplomasia kati ya viongozi wakuu wa Kore Kaskazini na mataifa mengine isipokua China na Urusi. Lakini katika utawala wa Donald Trump alijaribu kukutanaa na Kim Jong Un karibu mara tatu huko Hanoi Vietnam, Singapore na katika mpaka wa Korea Kaskazini na Korea kusini kati ya 2018-2019. Ijapo hakuna kilichotokea baada ya mikutano hii. 

HII NDIO HATARI KAMILI KATIKA VITA HUKO UKRAINE. VITA YA TATU YA DUNIA AU VITA VYA NYUKLIA

Image
Picha ya pamoja ya viongozi wa Ulaya na Rais wa Marekani ikulu ya Marekani tarehe 18 Agosti 2025. Picha na AFP  February 2022 Urusi iliivamia Ukraine kijeshi katika kile ambacho Moscow walikiita kama Operesheni Maalumu  (Special Operation). Na tangu wakati huo vita hio imeendelea na dalili za kukoma kwake bado zinaonekana ziko mbali kulingana na matokeo ya jitihada mbalimbali za kukomesha vita hivyo. Lakini kwa sasa vita vimeingia katika hatua muhimu na huenda ni hatua mbaya sana ambayo kosa kidogo la kimahesabu limaweza kuigharimu dunia kama ilivyokua Julai 1918 au Septemba 1939 ambapo vita vya kwanza na pili vilianza mtawalia. Kwa sasa vita vya Ukraine vina sura ya tofauti ambayo inahatarisha usalama wa dunia. Na haya ndio mambo ya hatari zaidi ambayo yanaweza kushindwa kuzuilika na kuleta vita ya tatu ya dunia.

VITA YA WAJUMBE VS KAMATI KUU YA CCM MWAGA MBOGA, NIMWAGE UGALI. MBUNGE WAKO ULIYEMTARAJIA YUKO SALAMA?

Image
Hatimae mchakato wa kuchuja majina kwa wagombea nafasi ya wagombea katika ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) umefikia tamati baada ya kamati kuu ya CCM hapo jana kuweza kupitisha majina ya wagombea wake katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyanyika mwezi Oktoba mwaka 2025. Katika mchujo huo kumeshuhudiwa mapinduzi baada ya majina ambayo wajumbe waliyakataa na katika ngazi ya taifa kamati kuu ya CCM yaani (NEC) imewarudisha tena kwa wananchi.  Bofya kwenye maandishi ya bluu (PDF) kusoma zaidi majina ya walioteuliwa kugombea 2025.  Majina ya waliopitishwa na NEC ya CCM kugombea ubunge 2025 Je mbunge wako uliyemtarajia "kaliwa kichwa" na kamati au wajumbe sasa ndiyo wameliwa kichwa? Tungefurahi kupata maoni yako.