Tuesday, 26 September 2023

CHINA NA MAREKANI: HISTORIA, UHASAMA NA TISHIO LA DUNIA-2

Volume 1

Issue 2 [Muendelezo]

2023/0/25 

Rais wa China Xi Jin Ping (kushoto) na Rais wa Marekani Joe Biden (kuliko)

China ni Taifa Jeuri na Kiburi Cha Kimya.

Ikiwa tunapaswa kuelewa majibu ya China dhidi ya Marekani basi hatuna budi kuangalia hatua mbalimbali ambazo Marekani iliwahi au imezichukua dhidi ya China katika nyanja zote za kiuchumi, kisiasa na kijeshi. Lakini tutaangazia zaidi hatua zilizochukuliwa katika miaka ya hivi karibuni.

Bado ni hoja nyepesi kusema kinachoendelea kati ya Marekani na China ni muendelezo wa vita baridi labda kwa asiyeifahamu vita baridi. Ilikua inatisha kuliko jina lake la ‘vita baridi’. Kuna mambo kadhaa yameweka reheni mahusiano ya China na Marekani na ni muhimu kuyaangazia kiasi.

Sunday, 24 September 2023

CHINA NA MAREKANI: HISTORIA, UHASAMA NA TISHIO LA DUNIA

 Volume 1 | Issue 1

2023/09/24

Meli ya kivita ya Marekani

Picha za mtandao


Historia ya Taifa la China.

Tofauti na Marekani, taifa la China lina umri mrefu sana. Uchina ya kale (“Ancient China”) imekuepo tangu miaka 2000 Kabla ya Kristo/ Kabla ya kipindi cha sasa (2000BC/BCE). Wakati huo Uchina ilikua imegawanyika katika koo mbalimbali kama Zhang, Zhou, Quin, Han na nyinginezo. Ugunduzi wa kale wa risasi, dira, maandishi na uchapaji vilianzia huku. Historia yake ni ndefu mno, hatutoweza kuiandika yote.