Volume 1
Issue 2 [Muendelezo]
2023/0/25
![]() |
Rais wa China Xi Jin Ping (kushoto) na Rais wa Marekani Joe Biden (kuliko) |
China ni Taifa Jeuri na Kiburi Cha Kimya.
Ikiwa tunapaswa kuelewa majibu ya China dhidi ya Marekani basi hatuna budi kuangalia hatua mbalimbali ambazo Marekani iliwahi au imezichukua dhidi ya China katika nyanja zote za kiuchumi, kisiasa na kijeshi. Lakini tutaangazia zaidi hatua zilizochukuliwa katika miaka ya hivi karibuni.
Bado ni hoja nyepesi kusema kinachoendelea kati ya Marekani na China ni muendelezo wa vita baridi labda kwa asiyeifahamu vita baridi. Ilikua inatisha kuliko jina lake la ‘vita baridi’. Kuna mambo kadhaa yameweka reheni mahusiano ya China na Marekani na ni muhimu kuyaangazia kiasi.