Posts

Showing posts from August 17, 2025

OPEN AI YAMKAANGA ELON MUSK NA MARK ZUCKERBERG HUKO MAHAKAMANI

Image
Sam Altiman muanzilishi na mkurugenzi mkuu wa Open AI. Picha na AFP na Getty Images  Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali nchini Marekani zinaonesha kua kampuni ya Open AI ambayo inamilki ChatGPT imetoa maelezo mahakamani kua tajiri namba moja duniani Elon Musk alijaribu kumshawishi hasimu wake kibiashara Mark Zuckerberg ambae ni mmiliki wa kampuni kubwa ya Meta (Facebook, Instagram, WhatsApp na Thread) ili wachanhiane au waingie ubia katika uwekezaji wa kuinunua Open AI ambapo Elon Musk aliweka dau la dola za kimarekani bilioni 97.4, hata hivyo kulinga na Open AI Zuckerberg hakua ameafiki hilo. 

KAMPUNI YA APPLE IMEISHIWA 'PAWA'. YAOMBA MSAADA KUTOKA GOOGLE

Image
  Picha kwa hisani ya mtandao/ Shutterstock   Kulingana na vyanzo mbalimbali vya habari nchini Marekani, Apple Inc ambayo ni kampuni kubwa ya utengenezaji wa vifaa vya kielekroniki kama vile simu za iPhone na  Laptop za MacBook wako katika mazungumzo na kampuni kubwa pia ya teknolojia ya Alphabet Inc ambao ndio wamiliki wa Google kuhusu uwezekano wa kampuni ya Google kupewa kandarasi ya kuunda mfumo wa akili unde (AI) wa Apple ambao utakaotumika kuendesha Program ya sauti ya Apple maarufu kama Siri ambayo kwa muda mrefu Apple wamekua wakijaribu kuiboresha lakini hakuna mafanikio makubwa kutokana na vikwazo vya kihandisi katika mfumo huo. Apple yuko nyuma ya Google na Samsung ambao wana programu bora kwa sasa. 

MAJARIBIO YA JESHI LA MAREKANI YAMEENDA NDIVYO SIVYO. HII NI MBAYA SANA.

Image
MAJARIBIO YA JESHI LA WANAMAJI WA MAREKANI LIMEENDA OVYO VIBAYA MNO. SIO DALILI NJEMA. Picha na Petty Officer 2nd Class Clayton/ Us military   Wanasema 'siku njema huonekana  tangu asubuhi 'lakini hii sio kwa Jeshi la Wanamaji la Marekani. Ikiwa ni miongoni mwa majeshi yenye nguvu zaidi duniani, mara zote hua liko mbele ya muda lakini kwa hiki kilichotokea hivi karibuni kinaacha maswali mengi miongoni mwa wataalam wa kijeshi.  Mwezi uliopita jeshi hilo lilikua likifanya majaribio ya boti zinazojiendesha zenyewe ambapo lengo kuu lilikua ni kua na kweza kua na uwezo wa kulidhibiti jeshi la wanamaji wa Jeshi la Ukombozi wa Watu wa China (PLA) ambalo kwa miaka ya hivi karibuni limeshuhudia maendeleo makubwa na ya haraka ya kimuundo, silaha na teknolojia. Sasa wakati wa majaribio hyo huko Pwani ya California kulitokea matukio yaliyotilia mashaka uwezo wa Jeshi la Marekani kumudu vita vya kisasa ambavyo vinahitaji teknolojia za kisasa zaidi na hilo tayari limegahrimu kazi za wa...

HATARI YA "AI" YA ELON MUSK: IMETOA SIRI JINSI YA KUMUUA BOSS WAKE ELON MUSK

Image
Picha kwa hisani ya mtandao/ Nacional.hr Kitu kikubwa kinachozungumzwa kwa sasa katika Ulimwengu wa teknolojia ni Akili unde au Akili mnemba maarufu kama Artificial Intelligence (AI). Makampuni makubwa kama Alphabet Inc. (Google) ,wana AI yao ambaayo ni Gemin AI, Microsoft wana Copilot, Open AI wana ChatGPT, xAI wana Grok, Meta wana Meta AI na pia kuna Deep Seek kutoka China. Kwa sasa biashara kubwa ni AI. Hakuna kampuni imekua ikitaka kua nyuma katika hili. Lakini kuna jambo moja kubwa la kitisha ambalo bado watumiaji hatuweza kuwekwa wazi juu ya dhamira halisi ya hizi akili unde na wengi wanatumia kwasabau zipo bila tahadhari. Lakini hivi majuzi kumeshuhudiwa mambo ya hatari ambayo Akili Unde imeweza kujaribu kufanya. 

BAADA YA MIAKA 113 KANISA LAHAMISHWA BILA KUVUNJWA.

Image
Kanisa la Lutheran la Kiruna huko Sweeden likiwa tayari kusafirishwa. Picha kwa hisani ya Forbes Katika hali ambayo sio ya kawaida kanisa moja la kihistoria huko nchini Sweeden limehamishwa kutoka sehemu mabo lilijengwa na kupelekwa sehemu nyingine baada ya miaka 113 la kuwepo katika eneo ambapo ujenzi wake ulikamilika mwaka 1912. Kuhamishwa kwa kanisa hilo la Lutheran ni kutokana na kuwepo kwa uchimbaji wa madini ya chuma chini ya kanisa hilo na maeneo mengine ya jirani. Mpango wa kuhamisha kanisa hilo bila kubomoa umekua ukiendelea kwa takribani mwaka mmoja ambapo wataalam wamekiri kwamba haikua kazi rahisi. 

WANAJESHI WA URUSI WAPEPERUSHA BENDERA YA MAREKANI KWENYE MSTARI WA MAPAMBANO HUKO UKRAINE

Dunia inastaajabisha sana na wakati flani matukio kadhaa yanaweza kuonekana kama mchezo wa kuigiza au mzaha lakini baadae hugeuka kua ni maisha halisi ya baadhi watu. Katika kisa kimoja cha kushangaza sana imetokea huko katika mstari wa mbele wa mapambano kati ya majeshi ya Ukraine na majeshi ya Urusi ambapo kifaru cha Marekani Armoured Personnel Carrier (APC)  kilioneka kikiwa mwendo huku kikiperusha bendera mbili nyuma. Moja ikiwa ni ya Urusi na nyingine ikiwa ni ya hasimu na adui namba moja wa Urusi ambaye ni Marekani. Hili halikutazamiwa kuona kwamba linatokea kwa sasa lakini limetokea na kupokelewa na ukosoaji mkubwa kutoka Ukraine wakilaani tukio hilo. Hayo ni kwa mujibu wa Russia Today (RT).

UMOJA WA ULAYA, UINGEREZA, NATO, TRUMP NA ZELENISKY WANAMKABIA JUU PUTIN, WATAWEZA?

Image
Kutoka kushoto ni Rais wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Layen, waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer, Rais wa Finland Alexander Stubb, Rais wa Ukraine Volodymr Zelenisky, Rais wa Marekani Donald Trump, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, waziri mkuu wa Italia Giorgina Meloni, Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz na katibu mkuu wa NATO Mark Rutte .  Huenda siku ya Jumatatu 18, 2025 ikawa miongoni mwa siku kubwa kabisa katika siasa za kimataifa na diplomasia. Misukosuko ya Ulaya inawaleta viongozi wa nchi kubwa za Ulaya pamoja na Ukraine nchini Marekani na wote wakisubiri kwa hamu kuweza kusikia kile ambacho Rais wa Marekani Donald Trump alikua akitazamia kuamua juu ya hatma ya vita vya Ukraine na zaidi ya yote juu ya hatma ya Ulaya na NATO. Mgogoro wa Ukraine ni mgogoro mbaya zaidi kwa Ulaya tangu kuisha kwa vita baridi mnano 1991. Wangeliweza kukaa na kusubiri Volodymr Zelenisky na Trump wajadiliane na wapewe mrejesho lakini kamwe hilo halikuonekana kutokea kwani wote wal...

DUNIA INAHAMIA WASHINGTON KWA MUDA: WASHINGTON NI YA MOTO

Image
DUNIA INAHAMIA WASHINGTON KWA MUDA: WASHINGTON NI YA MOTO Rais wa Ukraine kushoto akifurahia na mwenyeji wake Rais Donald Trump wa Marekani, ikulu ya White House Agosti 18, 2025. Picha na Reuters Leo jijini Washington inatazamiwa kua ni moja kati ya nyakati ngumu na muhimu zaidi tangu vita vya Pili vya dunia vilivyomalizika mwaka 1945. Wakati kulishuhudiwa nyakati ambapo viongozi wengi wa dunia wapishana katika makao makuu ya nchi kama kubwa au miji iliyokua na ushawishi kama vile Potsdam huko Ujerumani na Yalta huko Crimea nchini Urusi.  Baadae Washington ikawa kitovu cha mikutano mikubwa ya kuamua hatma ya siasa na maendeleo ya dunia kwa kua miji ya Ulaya kama vile Berlin, Brussels, Vienna na London ilikua imepoteza ushawishi wake. Na Washington imebakia kama kielelezo cha Ushawishi duniani ambapo viongozi mbalimbali hukutana. 

AFRIKA NI KUBWA KIASI GANI? KWANINI SASA WAAFRIKA WANADAI RAMANI HALISI?

Image
AFRIKA NI KUBWA KIASI GANI? HATIMAYE AFRIKA IMEANZA KUZINDUKA. Ramani ya dunia  Tulipokua shuleni tulijifunza mengi juu ya Afrika lakini mengi ilikua ni upotoshaji wa kukusudia au kutokukusudia. Hilo linajidhihirisha pale unapotazama ramani ya dunia. Utaambiwa Afrika ni bara la pili kwa ukubwa duniani nyuma ya Asia lakini ukitazama ramani utagundua Amerika ya Kaskazini inaonekana kuwa ni kubwa kuliko Afrika. Lakini je Afrika ina ukubwa gani? Na kwanini sasa Umoja wa Afrika unahitaji taasisi kuu ulimwenguni kote kutumia ramani mpya ya Afrika kulikoni?  Tunarejea takribani miaka 456 hivi nyuma kuanzia sasa. Tunakutana na mwaka 1569, na hapo tunakuja kukutana na mtu mmoja aliyepata kua ni mwanajiografia na mchora ramani kutoka Flanders (Kijiografia eneo hili liko Ubelgiji na kijamii na kiutamaduni limekaliwa na watu asili ya Wadachi). Mtu huyu alitwa Gerardus Mercator ambaye ndiye aliyechora ramani hii ya dunia ambayo katika karne ya 18 ilirasmishwa kutumika katika maswala ya usa...

TRUMP VS PUTIN NANI MBABE WA MWENZAKE?

Image
TRUMP VS PUTIN NANI MBABE WA MWENZAKE?   Rais wa Marekani Donald Trump akiongea jambo na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin baada ya mkutano wao huko Alaska 15 Agosti 2025/ picha kwa hisani ya Ikulu ya Marekani   Rais wa Marekani Donald T rump na Rais wa Urusi Vladimir Putin ni miongoni mwa majina makubwa katika medani ya siasa za kimataifa kutokana na hulka yao na namna wanavyochukua maamuzi magumu katika nyakati ngumu. Na hivyo kufanya dunia kua na viongozi shupavu kama wanne hivi kwa maana ya nyongeza ya Xi Jin Ping wa China pamoja na Kim Jong Un wa Korea Kaskazini. Ila kwa sasa ni Trump dhidi ya Putin wakikaa wawili nani mbabe wa mwenzake?