Monday, 20 November 2017
SAWA, HATIMAE MUGABE AKUBALI KUJIUZULU.
Kwa mujibu wa taarifa ya CNN imeripoti kua chanzo rasmi kinachofuatilia mazungumzo kati ya rais Mugabe na maafisa wa jeshi kimedokeza kua rais Mugabe amekubali kujiuzulu kufuatia hatua ya vikosi vya jeshi la nchi hiyo kumuweka kizuizini kwa siku kadhaa. Hatua hii inakuja kufuatia hatua yake ya jana jumapili ambapo kwa mara ya kwanza tangu awekwe kizuizini nyumbani kwake alilihutubia taifa kupitia shirika la utangazaji la nchi hio ZBC.
Sunday, 19 November 2017
MUGABE ATIMULIWA UENYEKITI WA ZANU-PF
Chama tawala cha ZANU-PF cha nchini Zimbabwe kimeridhia kumuondoa Robert Mugabe kama mwenyekiti wake na kumteua aliyekua makamu wake wa rais Emmerson Mnangagwa kua mwenyekiti mpya wa chama hicho. Mnangagwa alifutwa kazi na rais Mugabe siku chache zilizopita na kutaka kumtangaza Grace Mugabe kua makamu wa rais na hatimaye aje kua mwenyekiti na baadae rais wa Zimbabwe kitu kilichoamsha hasira na sintofahamu miongoni mwa wazimbabwe wengi.
Hatua hio ilimlazimu generali wa jeshi la zimbabwe (ZDF) Gen Constantino Chiwenga kutangaza kuingilia kati mzozo huo siku ya jumatatu na siku ya jumatano vikosi vya jeshi kulazimika kuchukua udhibiti wa serikali kwa kumuweka kizuizini rais Mugabe na kutaka atangaze kuachia madaraka hatua iliyosimamiwa na kanisa katoliki lakini taarifa zilidai kua Mugabe alikataa kufanya hivyo na pia vilizingira kituo cha habari cha ZBC.
Hata hivyo leo chama hicho tawala kimeamua kumvua uongozi mwenyekiti wake Robert Mugabe 93, pamoja na mkewe Grace Mugabe ambaye ametimuliwa kabisa ndani ya ZANU-PF. Msafara wa magari ya rais ulionekana ukipita barabarani ukitokea kwenye nyumba la Mugabe japo haikuthibitika mara moja kama rais Mugabe alikuwapo ndani kwenye msafara huo.
UTUMWA BADO UNAITESA DUNIA YA TATU
Wakati dunia ikifurahia na kusherehekea mafanikio mengi na hatua kubwa iliyofikiwa na binadamu, hii sio habari na sio furaha ya kila mtu. Ni wakati ambao baadhi ya jamii zinataabika kwa mabalaa ya umaskini uliokithiri, njaa kali, majanga ya asili na vita vya wenyewe kwa yenyewe na kubwa zaidi ni SULUBU YA UTUMWA!
Subscribe to:
Posts (Atom)