Wednesday, 30 September 2020

DALILI ZA SIRI AMBAZO ZINAASHIRIA MWILI WAKO HAUKO SAWA.


 

Wakati flani sote hua tunaamini kwamba tuko bukheri wa afya njema kabisa, lakini kwa kiasi kikubwa bado tunaweza kua sio sahihi. Swala la kuhakikisha unakua na afya njema ni la msingi kabisa na ni lazima lipewe kipaumbele. Kuna dalili kadhaa ambazo mwili huonesha lakini wengi wetu huzipuuzilia mbali kwani hua hawaoni kama dalili hizo hazina madhara makubwa kwenye afya yao. Lakini ukweli ni kwamba dalili ndogondogo zina maana kubwa kwa afya yako hivyo basi chukulia tahadhari na umakini mkubwa kuhusiana na vitu hivyo vidogo vidogo zinavyotokea katika mwili wako. Hizi baadhi ya dalili za siri zinazoashiria hauko sawasawa kiafya.