HAMAS: KUTOKA KIKUNDI CHA KUTOA MISAADA MPAKA KIKUNDI CHA KISIASA NA KIJESHI.
Ili kuelewa
imani na itikadi kali ya Hamas kabla hata kuundwa kwake tuone kidogo ikitikadi ya
Waarabu juu ya taifa la Israel hasa kabla ya vita vya siku sita [5-11 June
1967]. Hizi ni kauli za kukupa picha HAMAS wanasimamia nini na Wanapigania nini.
Radio
Cairo ilitangaza kua "[Watu] Waarabu wamedhamiria kikamilifu kuifuta
Israel katika ramani na kirejesha heshima ya watu wa Palestina". May 25,
1967.
May
28, 1967 rais wa Misri Gamal Abdel Nasser anasema "Hatutakubali uwezekano wowote ule wa
Israel na Palestina kuwepo pamoja".
31
May 1967 rais wa Iraq Abdel Rahman Aref anasema "Uwepo wa Israel ni dosari
ambayo ni lazima irekebishwe".
Utaona
msimamo mkali wa Waarabu dhidi ya Israel kwa hio salama ya Israel ilikua ni
kupitia kujua namna gani atakua wa kwanza kujilinda dhidi ya maadui zake ambao
wote wanatangaza kumuangamiza.
Sasa
kwanini HAMAS ilianzishwa turudi 29 August 1967 kule Khartoum Sudan kulikaliwa
mkutano wa Shirikisho la nchi za Kiarabu (Arab League) iliokua na makao makuu
pale Cairo, Misri. Katika kilele cha mkutano huo Arab League ilikuja na azimio
la HAKUNA/HAPANA TATU (THREE NOES) ikiwa ni No peace with Israel, No
recognition of Israel na No negotiation with Israel [ Hakuna amani na Israel,
Hakuna kuitambua Israel na Hakuna majadiliano na Israel]. Na hili linaanzia
katika imani ya Waarabu hata kabla ya vita mfano tizama msimamo wa Misri na
Iraq kabla ya June 5, 1967.
:::::::::::::***
Vita
vya siku sita mwaka 1967 vinahitaji muda kujadili lakini matokeo kifupi vita
viliisha kwa aibu kubwa mno kwa Waarabu. Lakini kwa Israeli iliwafanya
wajipatie maeneo mengi zaidi kama Golan Heights kkutoka Syria, East Jerusalem kutoka
Jordan, Ukingo wa Gaza na Sinai. Jumla ya maeneo haya ilikua ni mara tatu ya
ukubwa wa Israel.
1973
tumeona katika sehemu ya pili kua Waarabu waliivamia tena Israel safari hii
hakukua na mshindi wa wazi. Israel na Misri chini ya Marekani zikaanza mchakato
wa amani. Mwaka 1978 wanakutana na kuafikiana baadhi ya mambo pale Camp David
nchini Marekani.
1979
Egypt anakua taifa la kwanza la kiarabu kuvunja kiapo cha Khartoum cha mwaka
1967 na anatimuliwa kutoka Arab League na makao makuu yanagamishiwa Tunis. Kifupi
ni kwamba Misri sio tu kama ilitengwa bali ilichukiwa na jumuiya nzima ya Kiarabu
na zaidi Wapelestina waliona wamesalitiwa na ndugu zao. Lakini chuki ikazidi zaidi
kwa Wayahudi wa Israel.
Fikiria
hili.
Hadi
hapo utagundua mtetezi mkubwa wa Palestina alikua ni Misri na sasa Misri
kasaini makubaliano ya amani na Israel. Je, nani alibaki kuwapambania Waarabu?
Ilikua hivi;
![]() |
Wapiganaji wa Hamas wakiwa na silaha |
KUANZISHWA
KWA HAMAS
1973
Imam mmoja kutoka Palestina alianzisha "Kituo cha Kiislamu" cha kutoa
misaada ya kijamii kiliitwa mujamah al-Islamiya. Kilifanya kazi kubwa kusaidia
watu. Mwaka 1987 kulizuka vurugu za Wapalestina zilizofahamika kama Intifada na
ndizo zilizoweka msukumo wa kubadilika kwa Islamic Centre hio (mujama al
Islamiya) kua Islamic Resistance Movement. Naam HMS inazaliwa chini ya Imam
Sheikh Ahmed Ismail Hassan Yassin.
1979
Egypt anakua taifa la kwanza la kiarabu kuvunja kiapo hicho na anatimuliwa
kutoka Arab League na makao makuu yanagamishiwa Tunis.
Ilikua
10 December 1987 ambapo Imam mmoja anaamua kubadili kikundi kimoja cha misaada
kua kundi la kiharakati na likaitwa Harakat al Muqawamah al-Islamiyyah [HAMAS]
ikiwa na maana ya Islamic Resistance Movement.
Kumbuka 8 December 1987 kuna vurugu zilianzishwa na Wapelestina
wakipinga mauaji ya wapalestina wanne katika ajali ambayo wao wanadai Israel
ilifanya makusudi kuwagonga hao Wapelestina kama kulipiza kisasi baada ya akari
mmoja wa Israel kuawa siku takribani mbili hivi kabla ya 8 December. Hizo vurugu
zinaitwa Intifada ya kwanza zilidumu kwa takribani miaka minne.
Hamas
walishikilia msimamo wa azimio la Khartoum baada ya kuona kuna namna viongozi
wa Palestina walikua wakiendekeza kutafuta suluhu ya amani na Israel. Kwa hio wao
waliamini namna pekee ya kuelewana na Israel ni kupitia vita ambavyo wanaamini wangeshinda
au watashinda.
Mfano
kulikua na jitihada za kujadiliana kati ya Palestinian Liberation Organization
(PLO) na Israel kule Oslo Norway. Majadiliano hayo yalifikiwa 1993 lakini
hakuna hatua iliyopigwa kuyafikia.
Majadiliano haya hayakuungwa mkono na HAMAS na wakabaki kua wapinzani
wakuu wa Israel. HAMAS WANATA VITA TU.
HAMAS
ikapata ufadhili kutoka mataifa kama Iran na Kuwait ikasukwa kwa kuunda mkondo
wa Kijeshi ambapo wana kikosi kinaitwa The Izz ad-Din al-Qassam Brigades
'Battalions of martyr Izz ad-Din al-Qassam'; au Al-Qassam Brigades chini ya
mwanajihadi maarufu na pasua kichwa kwa Israel kwa sasa ambae ni Mohammed Deif.
Mpaka sasa kwa taarifa za CIA World Factbook Hamas inawaoiganaji kati ya 20,000-
25,000.
Mwaka
2000 waziri mkuu wa Israel Shimon Perez alitembelea Al Aqsa sehemu ya tatu kwa Utakatifu katika dini ya Kiislam.
Wapelestina wakaanzisha vurugu ambazo zilikuja kua Intifada ya pili baada ya
ile ya 1987. Sasa pia kutokana na asili ya eneo la Jerusalem pia Israel huenda imekua
ikifanya machukizo dhidi ya Waislam hivyo kuundeleza uhasama baina yao.
Ukiachilia
mbali kwamba wanahimiza vita dhidi ya Israel kumbuka pia wana tawi la kisiasa.
Jeshi la Israel liliondoa kikamilifu vikosi vyake Gaza na kuikabidhi Gaza kwa
Mamlaka za Palestina kujitawala ikiwa ni utekelezaji wa makubaliano ya Oslo ya
1993.
Sasa
Hamas walikua na nguvu upande wa Gaza na katika uchaguzi wa Palestina wa 2006
walipata kura nyingi Gaza na hivyo kuunda serikali yao mwaka 2007. Lakini pia wana wafuasi wengi katika ukingo
wa Magharibi (West Bank). Kuanzia 2007 mpka leo hakujawahi kua na mahusiano
mazuri kati ya Gaza chini ya HAMAS na Israel ambayo inaitambua HAMAS kama
kikundi cha Ugaidi. Kwa hio baada ya hapo Israel imekua ikihofia usalama wake
hasa kutoka Gaza ambako Hamas wanatawala.
WATU
TOFAUTI, ITIKADI TOFAUTI ILA LENGO MOJA.
HAMAS
vs ISRAEL kitu cha kwanza kuelewa ni kwamba wote wana uchu uliopitiliza wa
ARDHI. Kwa hio ni vita ya nani ana haki ya eneo ambalo sasa ni nchi ya Israel.
HAMAS wanalitaka na ISRAEL wanalitaka na wamelishikilia. HAMAS hawako tayari
kugawana eneo na Israel wako tayari kuongeza hata nchi moja katika ukingo wa Gaza
kwa maana watafuta dhana ya Israel ya Waisrael ikibidi ila hawako tayari
kupunguza hata kwa sentimita moja eneo lolote la Israel.
Suala
la dini linatumika kutengeneza itikadi ya mapambano ila sio sababu ya kwanza
kasoro tu linapokuja swala la Jerusalem ambapo kila mtu anautaka mji lakini ni
kwa sababu za kiunabii na hofu ya labda ukweli wa kuogofya. Kwa maana Wayahudi,
Wakristo na Waislamu wote wanautumia mji huo kama mji mtakatifu. Mwaka 1947 wakati
wa kuigawa Palestina, Umoja wa Mataifa (UN) ulipanga utakua mji huru si Israel wala
Palestina alopaswa kuudhibiti lakini kwa sasa Jerusalem yote iko chini ya Israel
na ndio makao makuu mapya ya Israel tangu 2018 lakini pia Wapalestina wanataka taifa
lao likiundwa basi Jerusalem uwe ndio mji mkuu wa Palestina.
Sera
za ubepari za kujitanua ni kikwazo kwa ustawi wa Wapelestina na itabakia
changamoto kubwa mashariki ya kati. Makazi ya Walowezi eneo la West Bank ambako
Israel imekiuka azimio la Umoja wa Mataifa la 1967 bado linawanyima usingizi
Wapelestina.
Na
mwisho ni kwamba kila upande unataka kuishi. Kwa hio kama HAMAS hatopambana
haki ya Palestina na watu wake inaweza kupotea kabisa sio tu kwa maana ya eneo
bali watu wake, utambulisho wao na jina Palestina pia litatoweka. Na endapo
Israel ikijisahau inaweza kusambaratishwa walau kwa muda. Hofu hii inafanya
Israel kutumia nguvu kubwa mno kupambana. Na inateswa na unabii katika nyakati
ambazo huenda ni sasa. Wanajaribu kuepuka hicho kinachosemwa kisitokee? Ikiwa
ndivyo, wanaweza kupinga unabii usitimie?
Unabii na Historia vimekua vikifanya mzozo huu kutokua na suluhisho kamilifu na thabiti na la mapema. Kwa Israel ni nchi ya ahadi kutoka kwa Mungu na kwa Palestina ni nchi waliyorithishwa vizazi na vizazi. Na vita hivi vitakuepo kwa muda mrefu. Sio vya kwanza na haviwezi kua vya mwisho.
Kwani
wana hakika kwamba Israel iliyosemwa ni hii ya kwao?
Tuchambue
nini tena?
Kwa maoni,
ushauri, maswali na majibu mengine zaidi unaweza kuwasiliana nami kupitia njia
zifuatazo.
Email:
karlrck@gmail.com
Phone:
0787505800
No comments:
Post a Comment