TRUMP APATA PIGO BAADA YA KUJIUZULU KWA MWENYEKITI WA KAMPENI.

Mwenyekiti wa kampeni ya Trump ajiuzulu


Mwenyekiti ya kampeni ya mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump amejiuzulu miezi miwili tu baada ya kushika usukani.
Alichukua nafasi hiyo kama mwenyekiti wa kampeni, baada ya meneja wa zamani Corey Lewandowski kufutwa kazi mwezi Juni.

Mtaalamu huyo wa masuala ya siasa wa umri wa miaka 67, amekuwa chini ya shinikizo kufuatia uhusiano wake na rais wa zamani wa Ukrain Viktor Yanukovych ambaye anaipendelea Urusi.
Lakini haijulikani ni kwa nini aliondoka kutoka kwa kundi hilo la kampeni lililofanyiwa mabadiliko wiki hii kwa kuongezwa meneja mpya pamoja na mkurugeni mkuu.
Bwana Manafort amekosolewa siku za hivi karibuni baada ya gazeti la New York times kuripoti kuwa serikali ya Ukrain ilifichua ahadi za kumlipa dola milioni 12 kwa kumfanyia kazi bwana Yanukovych.

Comments

Popular posts from this blog

HII NDIO HATARI KAMILI KATIKA VITA HUKO UKRAINE. VITA YA TATU YA DUNIA AU VITA VYA NYUKLIA

TOP 10 YA SIMU ZENYE KAMERA BORA ZAIDI DUNIANI MPAKA SASA

AFRIKA NI KUBWA KIASI GANI? KWANINI SASA WAAFRIKA WANADAI RAMANI HALISI?