Posts

WAAFRIKA WAUNGANA NA KUFANYA MAANDAMANO MAKUBWA NCHI GHANA. UMAJUMUI WA AFRIKA UNAPATA NGUVU MPYA?

Image
Moja kati ya bango likiwa na ujumbe kua "HATUDAIWI, HATUTOLIPA"  Bara la Afrika ni moja ila ikiwa Waafrika ni wamoja ni swali pana sana na inaweza kua vigumu  kufikia hitimisho la pamoja. Wakati wa Karne ya dhahabu kwa nchi za kiafrika naweza kusema ilikua ni kipindi cha miaka ya 1960s. Hapa tulishuhudia miito mbalimbali ya Waafrika kuungana na kua wamoja au kitu kimoja na  mwaka 1963 viongozi wa nchi huru za Afrika walifanikiwa kuunda Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) lakini baadae mwaka 2002 Umoja wa Afrika (AU) ulianza rasmi baada ya Sirte declaration kule Linya mwaka 1999.  Lengo lilikua ni kuwaleta Waafrika pamoja na kupigania haki na usawa katika nyanja za kimataifa. Kupitia mikutano na makongamano mbalimbali imekua dhahiri kua Afrika ina hitaji ukombozi mpya kwani sasa inaelekea kulekule tuliko toka kwenye miaka ya 1980s ambapo madeni ya nje yalizidhoofisha nchi za kiafrika na kufikia hatua ya kufilisika ndipo taasisi za kifedha za kimataifa na nchi wakopesha...

TRUMP NA MAREKANI VS NICOLAS MADURO NA VENEZUELA, JE, VITA IKO KARIBU?

Image
Rais wa Venezuela Nicholas Maduro. Picha na Reuters  Kumekuwapo na sintofahamu kubwa juu ya kile kinachoendelea kati ya Marekani na Venezuela kufuatia matendo hatarishi ya pande zote mbili. Awali Marekani ilitangaza dau nono la dola milioni 50 ambazo ni sawa na karibu sawa na shilingi 12, 529, 390, 000/= kama zawadi kwa mtu yeyote anatakaye wezesha kupatikana na kukamatwa kwa Rais wa Venezuela ambae anatuhumiwa kwa ulanguzi wa madawa ya kuelevya. Lakini hilo limechukua sura mpya baada ya Marekani kutuma meli za kivita pamoja na nyambizi karibu na Venezuela kitu ambacho kimemlazimu Rais Maduro kuanza kukusanya wanajeshi wakijiandaa kwa makabiliano ikiwa Marekani itawavamia. 

UEFA IMEFANYA MABADILIKO YA MUDA WA KUCHEZA SIKU YA FAINALI

Image
Shirikisho la mpira barani Ulaya linalosimamia mashindano ya Ligi ya mabingwa Ulaya kwa maana ya UEFA wametangaza mabadilko katika muda wa mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kuanzia msimu huu ya 2025/2026 ambayo itachezwa pale katika uwanja wa Puskas huko Budapest nchini Hungari. Mabadiliko haya ya muda yanafuatia tathmini ambayo UEFA wameifanya na kuamua kuweza kuwapa burudani mashabiki ambao hapo awali wamekua wakisumbuka kutokana na mechi baadhi kuchelewa kuisha hasa pale michezo hiyo inapoenda katika muda wa nyongeza na mikwaju ya penati. 

TOP 10 YA SIMU ZENYE KAMERA BORA ZAIDI DUNIANI MPAKA SASA

Image
Picha za smartphone mbalimbali Miongoni mwa masoko magumu kwa sasa ni pamoja na soko la simu janja au rununu (smartphones) ambapo kila kampuni ya utengenezaji wa siku inajitajidi kutoa simu zenye ubora wa hali ya juu. Lakini sio rahisi kama unavofikiria ikiwa utaulizwa ipi ni simu bora kwa sasa sokoni. Kwa sababu simu moja kutoka kampuni flani inaweza kua bora kwenye eneo moja au mawili hivi lakini ikashindwa kua bora katika maeneo mengine. Lakini kati ya vitu virahisi na hua ni kigezo cha watu kununua simu hua ni kamera. Hii hapa ni orodha ya simu 10 zenye kamera bora sana mpaka sasa. 

IRAN NA ULAYA ZAINGIA KATIKA MZOZO MPYA HUKU MAREKANI IKITAJWA PIA.

Image
Kiongozi mkuu wa taifa la Iran Ayatollah Ali Khamenei. Picha na New York Times Ni takribani miezi miwili imepita tangu kumalizika kwa vita vya siku 12 kati ya Israel na Iran. Katika vita hivyo ilishuhudiwa pia Marekani akiingilia kati kwa kuvishambulia vinu muhimu ya Nyuklia vya Iran ikiwemk kile kinu kikubwa zaidi cha Fordow, Nantaz na Isfahan tarehe Juni 22, 2025 ambapo mashambulizi hayo yaliibua hisia mseto kutoka katika Jumuiya ya kimataifa. Kufuatia mashambulizi hayo Trump alisema wameharibu kabisa uwezo wa Nyuklia wa Iran na kwamba huo ulikua ni ushindi mkubwa sana kwa usalama wa dunia. Lakini kauli ya Trump inapingana na ripoti ya shirika la ujasusi wa kiusalama lililo chini ya Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) yaani Defense Intelligence Agency(DIA). Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali ambayo kulingana na unyeti wa taarifa hawakutaka kutajwa walisema mashambulizi katika vinu vya nyuklia huko Iran vilirudisha nyuma mpango wa Nyuklia wa Iran kwa miezi kadhaa tu nyuma. Wakiamini ...

YOUTUBE ILITUMIA AKILI UNDE (AI) KUHARIRI VIDEO ZA WATU KWA SIRI

Image
Picha na AFP/Getty Images  Akili unde (AI) kama inavyofahamika imekua ni mapinduzi makubwa katika sayansi na teknolojia na kwa sasa ni ngumu kuwaza dunia bila Akili unde. AI sasa hivi inatumika katika tafiti za kisayansi, elimu, afya, viwandani, mtandaoni na karibu kila nyanja ya maisha ya binadamu kuna matumizi ya Akili Unde (AI) kwa kiasi fflani. Licha ya kua na fursa nyingi bado AI imeacha mwanya wa changamoto hasa zile zinazohusu hatimiliki na uhalisia wa mawazo au ubunifu kwani kam kitu au wazo litku limesanifiwa na akili unde ni ngumu kudai kwamba ni wazo lako licha ya kwamba uliielekeza namna ya kufanya. Katika changamoto mojawaponkubwa sasa inaikumba kampuni ya Google kupitia bidhaa yake ya YouTube.

MAANDAMANO MAKUBWA HUKO ISRAEL KUMSHINIKIZA NETANYAHU KUMALIZA VITA

Image
Mtu akionekana kuvuka barabara ambapo matairi yalichokwa moto siku ya maandamano Jumanne 26 Agosti 2025. Picha na Times of Israel/Idit Avishay/Pro Democracy Protest Movement  Maandamano makubwa yamefanyika leo kote  nchini Israel ambapo waandamanaji wamezuia barabara zote muhimu katika jiji la Tel Aviv wakiwa na lengo la kuishinikiza serikali ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kukomesha vita huko ukanda wa Gaza na kuweka kipaumbele kuachiwa kwa mateka wa Israel ambao bado wangali wanashikiliwa na wanamgambonwa Hamas huko Gaza. Maandamano hayo yamendaliwa na kuratibiwa na Hostages and Missing Families Forum.  Waziri mkuu wa Israel anakaniliaa na shinikizo kubwa la umma kufuatia vita ambavyo ukomo wake bado haufahamiki huko Gaza. Hayo yanajiri huku pia kukiwa na msukumo wa jumuiya ya kimataifa wa kumtaka Netanyahu kuamaliza vita vya Gaza vilivyodumu kwa takribani miezi 22 hadi sasa. Jana serikali ya Israel ilikuri kufanya shambulizi katika hospitali ya Nasser huko Gaza ambap...