KUMBUKIZI YA KIFO CHA GADDAFI.
Ilikua huko
katika mji wa Sirte alizaliwa mwana wa kiume kama Muammar Mohammed Abu
Minyar al-Gaddafi na baadae alifahamika kama Colonel Muammar Gaddafi kiongozi wa
Libya kati ya September 1, 1969-October 20, 2011. Alikua ni Mlibya
mmoja mwenye asili ya kitaliano aliyezaliwa na kukuzwa katika mazingira
ya kimaskini katika nchi maskini ya Libya.
Muammar Gaddafi
alibahatika kwenda shule huko Sabha na baadae alienda kujiunga na Royal
Military Academy huko Bengazi. Akiwa huko basi alianzisha kikundi chake chake kimapinduzi kilichokuja kufanya mapinduzi ya Libya. Huko pia alikuza falsafa zake
zilizoshabihiana na zile za vuguvugu la kujenga utaifa ndani ya nchi za
kiarabu (Arab Nationalism).
Muammar Gaddafi alialikua ni kiongozi wa Libya na alipata
uongozi baada ya mapinduzi ya mwaka 1969 akiwa kijana mdogo wa miaka 27
pekee aliyekua kanali wa jeshi la Libya. Aliupindua utawala uliopigiwa
chepuo na mataifa ya kibeberu kama Marekani, Ufaransa na Uingereza
uliokua chini ya Mfalme Idris I.
Akiwa mdogo Gaddafi alikua mtu
makini japo mda mwingi aliutumia akiwa mwenyewe akifanya mambo yake ya
msingi. Baada ya kumpindua mfalme Idris I, Gaddafi aliibadili Ufalme wa
Libya kua Jamhuri ya Libya Jamahiriya (1977) na alikua muumini wa
falsafa ya tatu ya kimataifa(The International Theory) ambayo ilipingana
na sera za kibepari na zile za Ukomunisti. Maendeleo mengi yalifikiwa
chini ya uongozi wa Muammar Gaddafi.
Ijapo hakua na mahusiano
mazuri mataifa ya magharibi hasa juu ya mpango wake wa nuklia ila
alifanikiwa kuiendeleza Libya licha ya vikwazo vya mabepari. Baada ya
George Bush kuivamia Iraq basi Gaddafi alihofia dhahma kama ile kua
ingemkumba na hivyo akaamua kuanzisha uhusiano mzuri na mataifa ya
magharibi kwa masharti kua ataondolewa vikwazo. Hayo yalifanyika mwaka
2004. Kuanzia hapo Libya ilistawi zaidi kutoka nchi maskini na kua nchi
ya kwanza kwa uchumi wa kichwa cha mtu mmoja mmoja.
Kwa mujibu
wa taarifa mbalimbali mpka Gadafi anauwawa Libya ilikua haidaiwi,
kulikua na huduma bure za kijamii, malipo kwa wasio na kazi na kiasi cha
fedha za mafuta wananchi walinufaika nazo moja kwa moja.
Licha
ya mafanikio haya, kuanzia mwaka 2010 kulikua na vuguvugu la mapinduzi
ya waarabu maarufu kama (Arab spring revolution). Mapinduzi hayaligusa
pia Libya vikosi kadhaa viliibuka na kuupinga utawala wa Kanali Muammar
Gaddafi. Baadae vikundi vya uasi vikafadhiliwa na nchi za magharibi chini wa mwamvuli wa Umoja kujihami wa nchi za magharibi wa NATO ili
kumuondoa Gaddafi madarakani. Aliapa kuilinda na kuitetea Libya mpka
mwisho na aliapa kwamba hatokimbia ila atafia Libya.
Baada ya
mapigano makali katika mji wa Benghazi na Tripoli, Muammar Gaddafi
alitaka kukimbilia katika mji wa Sitre alikozaliwa. Safari ile inakua ni
sehemu muhimu katika utawala wa Kanali Muammar Gaddafi na historia ya
Libya kwa ujumla. Akiwa njiani kuekea Sitre msafara wake ulishambuliwa
na waasi wakisaidiwa na ndege zisizokua na rubani (Drones). Alipojua kua
hawezi kukimbia aliingia na kujificha mtaroni ambapo waasi walifanikiwa
kushika.
Aliteswa sana, alilia sana na kati ya maneno
aliyoyaongea yalikua ni "kwani nimewakosea nini"?. Aliuliza hivyo kwa
kua alifanya yote kwa walibya kasoro UHURU tu ndio walikua hawana. Baada
ya mateso kadhaa inasemekana alipigwa risasi ya tumbo kwa mujibu wa
ripoti ya daktari. Lakini ripoti ya Umoja wa Mataifa (UN) ya mwaka 2012
inasemekana alijeruhiwa na bomu la kurusha kwa mkono kutoka miongoni wa
walinzi wake ambaye alijaribu kurusha bomu lakin likagonga kwenye ukuta
na kurudi.
Inasemekana pia mazishi yake na mwanae yalifanyika
tarehe 25 October 2011 katika eneo lisilofahamika huko jangwani. Huo
ukawa mwisho wa COLONEL MUAMMAR GADDAFI mwana wa Afrika. Afrika tuna mengi ya kujifunza kupitia Muamar Gaddafi.
Comments
Post a Comment