MWALIMU MKUU/ HEADMASTER SEHEMU YA TATU Baadae nilimskia mwalimu mkuu kua anataka kupumzika...kila mwamafunzi alifurahi kwa kua aliamini atasoma kwenye shule aliyokua akiiota.. Endelea...
Picha za smartphone mbalimbali Miongoni mwa masoko magumu kwa sasa ni pamoja na soko la simu janja au rununu (smartphones) ambapo kila kampuni ya utengenezaji wa siku inajitajidi kutoa simu zenye ubora wa hali ya juu. Lakini sio rahisi kama unavofikiria ikiwa utaulizwa ipi ni simu bora kwa sasa sokoni. Kwa sababu simu moja kutoka kampuni flani inaweza kua bora kwenye eneo moja au mawili hivi lakini ikashindwa kua bora katika maeneo mengine. Lakini kati ya vitu virahisi na hua ni kigezo cha watu kununua simu hua ni kamera. Hii hapa ni orodha ya simu 10 zenye kamera bora sana mpaka sasa.
Moja kati ya bango likiwa na ujumbe kua "HATUDAIWI, HATUTOLIPA" Bara la Afrika ni moja ila ikiwa Waafrika ni wamoja ni swali pana sana na inaweza kua vigumu kufikia hitimisho la pamoja. Wakati wa Karne ya dhahabu kwa nchi za kiafrika naweza kusema ilikua ni kipindi cha miaka ya 1960s. Hapa tulishuhudia miito mbalimbali ya Waafrika kuungana na kua wamoja au kitu kimoja na mwaka 1963 viongozi wa nchi huru za Afrika walifanikiwa kuunda Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) lakini baadae mwaka 2002 Umoja wa Afrika (AU) ulianza rasmi baada ya Sirte declaration kule Linya mwaka 1999. Lengo lilikua ni kuwaleta Waafrika pamoja na kupigania haki na usawa katika nyanja za kimataifa. Kupitia mikutano na makongamano mbalimbali imekua dhahiri kua Afrika ina hitaji ukombozi mpya kwani sasa inaelekea kulekule tuliko toka kwenye miaka ya 1980s ambapo madeni ya nje yalizidhoofisha nchi za kiafrika na kufikia hatua ya kufilisika ndipo taasisi za kifedha za kimataifa na nchi wakopesha...
Picha na AFP/Getty Images Akili unde (AI) kama inavyofahamika imekua ni mapinduzi makubwa katika sayansi na teknolojia na kwa sasa ni ngumu kuwaza dunia bila Akili unde. AI sasa hivi inatumika katika tafiti za kisayansi, elimu, afya, viwandani, mtandaoni na karibu kila nyanja ya maisha ya binadamu kuna matumizi ya Akili Unde (AI) kwa kiasi fflani. Licha ya kua na fursa nyingi bado AI imeacha mwanya wa changamoto hasa zile zinazohusu hatimiliki na uhalisia wa mawazo au ubunifu kwani kam kitu au wazo litku limesanifiwa na akili unde ni ngumu kudai kwamba ni wazo lako licha ya kwamba uliielekeza namna ya kufanya. Katika changamoto mojawaponkubwa sasa inaikumba kampuni ya Google kupitia bidhaa yake ya YouTube.
Comments
Post a Comment